Timu ya wekundu wa msimbazi Simba SC jana imezidi kujiongezea pointi 3 muhumu baada kuichapa timu ya Mtibwa SC bao 1-0 katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.Timu hizo zilicheza katika kipindi cha kwanza hadi kwenda mapumziko bila kufungana. Zilipo ingia kipindi cha pili timu hizo zilianza kwa kushambuliana na baadae dakika chache kabla ya mpira kumalizika mnamo dakika ya 92 ya nyongeza baada ya kuisha kwa dakika 90,timu ya Simba ilijipatia bao lake la ushindi kupitia kwa mshambuliaji wake wa kimataifa na raia wa Uganda EMMANUEL OKWI. Okwi aliifungia timu yake dakika ya 92 dakika 3 kabla ya mchezo kumalizika na kuwafanywa wapinzani wao Mtibwa kubaki wameduwaa na kumuona kama mwiba mchungu na kuwafanya mashabiki wao kutoka na furaha uwanjani hapo.Nayo timu ya Mtibwa sukari ilimpongeza Okwi lakini haikufurahishwa na maamuzi ya marefarii na kusema hawakutenda haki katika mchezo huo kwani wamekuwa wakiibeba sana timu ya Simba.